Tuesday 30 May 2017

Ernesto Valverde kocha mpya Barcelona

Ernesto Valverde
Klabu ya Barcelona imemtanga rasmi kocha wa zamani wa Athletic Bilbao Ernesto Valverde kuwa kocha wao mkuu mpya
Valverde ambaye ni mshambuliaji wa zamani wa Barcelona,wiki iliyopita  alitangaza kuwa anaondoka Athletic baada ya kudumu klabuni hapo kwa takriban miaka minne.
Meneja huyo, mwenye umri wa miaka 53, atamrithi Luis Enrique, ambaye alitangaza tangu mwezi Machi mwaka huu kwamba anaondoka Barcelona baada ya mkataba wake wa miaka mitatu kumalizika.

No comments:

Post a Comment