Monday 15 May 2017

Hans Poppe :Huu ni wakati wa kusonga mbele

Zacharia Hans Poppe, amereja Simba.
Uamuzi wa Hans Poppe kurejea Simba umetokana na mkutano uliofanyika hadi saa 9 usiku wa kuamkia leo.
Hans Poppe amethibitisha kurejea kwake kundini baada ya mkutano huo na viongozi.
Hans Poppe aliamua kujiondoa katika kamati ya utendaji ya Simba na akawa akawa ametoka kwenye kamati ya usajili aliyokuwa mwenyekiti.
Lakini kikao hicho hadi saa 9 alfajiri usiku wa kuamkia leo, kimemaliza suala hilo na Hans Poppe ameamua kurejea.

“Kweli tumekutana hadi saa 9 usiku, mwisho tumekubaliana na tumeyamaliza vizuri. Huu ni wakati wa kusonga mbele,” alisema Hans Poppe.

No comments:

Post a Comment