Shule ya Umwani ya CCM yachukuliwa na Serikali

"Bahati nzuri au bahati mbaya mimi ndiye Mwenyekiti wa CCM, natambua ile
shule ya Umwani ni ya CCM, sasa naagiza iwe ya Serikali.
Na Profesa Ndalichako yupo hapa ahakikishe masaula yote pamoja na madai
ambayo shule wanadaiwa na Jumuiya ya Wazazi yalipwe na shule irudishwe
serikalini.
Walimu na Wanafunzi wote watabakia pale pale na watakuwa ni wa serikali
wawe wameshindwa au kushinda mitihani yao." Rais Dk Magufuli, Bukoba.
Hayo ni maneno ya Rais Magufuli mapema leo Januari 2, 2017 alipokuwa
akiongea na wakazi wa Bukoba ikiwa ni sehemu ziara ya siku mbili mkoani
Kagera.
No comments:
Post a Comment