Friday 20 January 2017

Muimbaji wa Brazil, Loalwa Braz amefariki Dunia

Image result for Loalwa Braz
Muimbaji wa Brazil, Loalwa Braz, aliyejipatia umaarufu kwa wimbo wake wa mwaka 1989 ‘Lambada’, amekutwa amefariki kwenye gari iliyoungua moto mjini Rio de Janeiro.
Mwili wa muimbaji huyo aliyekuwa na miaka 63 ulikutwa karibu na nyumbani kwake huko – Saquarema.
Polisi bado hawajaweza kutambua sababu ya kifo chake.
Braz alikuwa muimbaji mkuu wa kundi Kaoma lililokuwa na makazi Ufaransa na Brazil na , lililopata umaarufu kwa wimbo Lambada. Msanii wa Marekani, Jennifer Lopez aliwahi kusample wimbo huo kwenye hit yake ya mwaka 2010, On The Floor.

No comments:

Post a Comment