
Kocha Jamhuri Kiwelu Julio,amesema
kwamba kwa sasa hana mpango wa kurejea katika kazi yake ya ufundishaji
wa mpira wa miguu hapa nchni kwa kuwa mpira wa Tanzania umetawaliwa na
siasa ambazo hazina msingi.

Julio amesema
kwamba licha ya kutakiwa na timu mbalimbali za hapa nyumbani,lakini
kwake hafikirii kabisa swala hilo kwani anaamini Tanzania hakuna watu
wanaofahamu vizuri uendashaji wa mpira wa miguu.
Amesema kwamba viongozi wengi ni
wababaishaji na wamejawa na majungu ambayo hayana msingi katika
uendelezaji wa mchezo huo unaopendwa Zaidi ulimwenguni.
Aidha amedai kuwa anaamini ipo
siku ataita waandishi wa Habari ili washuhudie jinsi atakavyochoma moto
vyeti vyake ili umma utambue kuwa dhamira yake ya kutofundisha soka iko
palepale wala sio jambo la mzaha.
No comments:
Post a Comment