Tuesday 24 January 2017

Zijue nchi ambazo zinalipa Wafanyakazi Mishahara mikubwa Duniani

Image result for dollar

 
1. USA
Pato la ndani kwa mwaka ni $55,000 na makato ya taxi ni asilimia 23.Wafanyakazi wa Marekani wanafanya kazi masaa 44 kwa wiki.

2. Luxembourg
Luxembourg ni wasambazaji wakubwa wa chuma ulaya. Kwa wastani kipato chao ni $38,951 kwa mwaka.

3. Norway
Norway ina utajiri mkubwa  wa maliasili ikiwa pamoja na mafuta,umeme wa maji,uvuvi na madini.Kwa wastani kipato chao ni $33,492 kwa mwaka.

4. Switzerland
Uswisi inashika nafasi za juu katika utendaji bora wa serikali yao, ikiwa ni pamoja na uwazi wa serikali yao, uhuru wa raia, ubora wa maisha, ushindani wa kiuchumi na maendeleo ya binadamu. Kwa wastani kipato chao ni $33,491 kwa mwaka na wanafanya kazi masaa 35 tu kwa wiki.

5. Australia
Australia ni moja kati ya nchi zenye uchumi imara zaidi duniani,ni wasafirishaji wakubwa wa madini na wanaagiza bidhaa chache sana kutoka nje.Katika swala la wastani wa utajiri, Australia ilishika nafasi ya pili duniani baada ya Switzerland mwaka 2013. Kwa wastani kipato chao ni $31,588 kwa mwaka baada ya makato yote ya kodi.

6. Germany
Germany ni nchi ya kwanza yenye uchumi mkubwa zaidi ulaya. Kwa wastani kipato chao ni $31,252 kwa mwaka baada ya makato yote ya kodi.

No comments:

Post a Comment