Tuesday 31 January 2017

Misikiti yafungwa nchini Uholanzi

Misikiti mikubwa yafungwa nchini Uholanzi
Misikiti mikubwa minne nchini Uholanzi yafungwa kwa muda baada ya tukio la shambulizi la msikiti mjini Quebec nchini Canada .
Kwa mujibu wa shirika la habari la Uholanzi ni kuwa baada ya shambulizi la Canada maafisa wakuu wa misikiti hiyo minne walifanya mkutano wa dharura .

Baadaye misikiti hiyo mikubwa iliyopo katika miji ya Amsterdam, Rotterdam, Hague na Utrecht ilitangazwa kufungwa kwa muda na kwa ajili ya usalama .
Takriban watu 6 walifariki baada ya watu 3 kuingia katika msikiti mmoja Canada na kushambulia waumini waliokuwa wanafanya sala ya usiku ,8 wameripotiwa kujeruhiwa katika shambulio hilo .

No comments:

Post a Comment