Wednesday 18 January 2017

Bunge la Gambia laongeza muhula wa Rais Jammeh

Yahya Jammeh aliingia madarakani kwa njia ya mapinduzi mwaka 1994Bunge la Gambia limeongeza muhula wa Rais wa Gambia Yahya Jammeh ambao unakamilika siku ya Alhamisi kufuatia kushindwa kwake kwenye uchaguzi kwa siku 90.
Bunge pia limeidhinisha uamuzi wa Jammeh wa kutangaza hali ya tahadhari ya siku 90, katika taifa hilo dogo la Afrika Magharibi.
Viongozi wa kanda wametishia kutumia nguvu za kijeshi kumlazimisha bwana Jammeh kuondoka madarakani, ikiwa atakataa kusalimisha mamlaka kwa rais mteule Adama Barrow.
Maelfu ya watalii raia Uingereza na Uholanzi wanaondolewa kutoka Gambia.
Nchi hiyo ni maarufu kwa watalii kutokana na fukwe zake.

Gambia ilitumbukia kwenye mzozo baada ya bwana Jammeh kukataa ushindi wa bwana Barrow kwenye uchaguzi wa tarehe mosi mwezi Disemba.
Viongozi wa kanda wameshindwa kumshawishi Bwana Jammeh kuwacha madaraka.

Nigeria imetuma meli ya kivita kumshinikiza bwana Jammeh kuondoka madarakani.
Muungano wa nchi za magharibi mwa Afrika Ecowas, umeandaa kikosi kinachoongozwa na Senegal lakini bado unasema kwa hatua za kijeshi ndizo zitakuwa za mwisho.

No comments:

Post a Comment