Tuesday, 10 May 2016

Ronaldo amefikisha Magoli 200 kucheza Michezo 171 kwa Misimu saba

 

 

 Na Kalonga Kasati

 Jina la Christiano Ronaldo si geni masikio mwa watu wengi wanaofuatilia soka uwezo wake katika kucheza Mpira na Mafanikio yake yalianza huko ureno na baadaye akahamia man United ambapo alipata umaarufu mkubwa sana katika

Ukijaaliwa kipaji, kinachofuata ni juhudi zako binafsi kuhakikisha unafikia malengo pia ukifikia malengo ya awali lazima ujiwekee malengo mapya. Kama ilivyokuwa kwa Cristiano Ronaldo, baada ya kutimiza malengo ndani ya Manchester United akaamua kutimkia Real Madrid ambako ametimiza malengo hadi yale ambayo hakuwa amejipangia.

Mfungaji bora wa muda wote Real Madrid  Cristiano Ronaldo amevunja rekodi nyingine akiwa santiago Bernabeu. Magoli aliyofunga jana dhidi ya Valencia yamefikia 200 akicheza katika dimba la SANTIAGO BERNABEU baada ya kucheza michezo 171 kwa misimu saba akiwa Hispania, Magoli 149 ameyafunga akiwa katika michuano ya ligi kuu Hispania wakati 40 akiyapata michuanao ya UEFA, mengine 10 yakipatikana kwenye kombe la mfalme yaani Copa de rey huku goli 1 likiwa Super cup.

Ronaldo ameanza safari yake ya kufunga katika uwanja huo akiifunga Deportivo. Lakini pia amefunga mabao mengi kwenye mchezo dhidi ya Granada alipopiga goli 5 peke yake msimu wa 2014/15. Mahesabu yanaonesha kasi ya Ronaldo ya kufunga ni goli 1.6 kwa kila mchezo.

Hapa Tanzania rekodi ya Mohamedi Hussein “Mmachinga” ya magoli 26 kwa msimu mmoja inabaki kuwa ngumu kuivunja wakati Ulaya kila mechi watu wanategemea kuvunja rekodi .

No comments:

Post a Comment