Hujuma za Baadhi ya Wafanyabiashara wa Sukari nchini

Na Kalonga Kasati
Nchini Tanzania makadirio ya Jumla ya
tani 590,000 za sukari zinahitajika, tani laki nne na Elfu ishirini
(420,000) kwa matumizi ya kawaida na kwa viwandani ni tani laki moja na
elfu Sabini (170,000), huku uwezo wa uzalishaji kwa viwanda vya ndani
ni tani laki tatu pekee, (300,000) kwa mwaka na kuacha pengo la mahitaji
ya tani laki mbili na elfu ishirini (220,000) Ambazo kimsingi inabidi
ziagizwe kutoka nje.
Mathalani ukiitazama nchi ya India,
kitunguu ni bidhaa muhimu sana kama Sukari Tanzania. Yaani ni karibia
kila mlo India wanatumia kitunguu. Kupanda kwa bei ya kitunguu India Mwaka 1980 kuliiangusha serikali madarakani na mwaka 1998 bei ya
kitunguu ndio iliamua Uchaguzi wa baadhi ya majimbo. Mwaka 2015 kitunguu
kilipanda tena na haraka serikali iliamua kuagiza kutoka Pakistani.
Tukirejea nchini Tanzania kuna viwanda
vinne (4) tu vinavyozalisha sukari navyo Ni Kilombero Sugar, TPC
Moshi, Mtibwa na Kagera. Ambapo makadirio ya mwaka kwa viwanda hivyo
ni;-
1.Kilombero Sugar (tani 120,000)
2.TPC Moshi ( tani 80,000)
3.Mtibwa (50,000)
4.Kagera (50,000)
Ni Dhahiri kwamba Tanzania
haijitoshelezi na wala haitajitosheleza kwa uzalishaji wa ndani wa
sukari kwa muda mfupi, isipokuwa pengo linazibwa na sukari kutoka nje,
hatua iliyomfanya Rais JPM kuamua kupiga marufuku uagizaji wa sukari nje
ya nchi ili itafutwe njia mbadala, ila wakati likisubiriwa hilo, imebaini vyanzo vya tatizo la upungufu wa sukari nchini humo.
1.Usafirishaji wa sukari kinyume na
sheria. Sukari zaidi ya tani elfu sitini (60,000) Husafirishwa nje ya
nchi bila kujali wakati wakijuwa kiwango cha sukari nchini hakitoshelezi
Mahitaji ya watumiaji.
2.Utoaji holela wa vibali. Utoaji
wa vibali ulikuwa holela kiasi kwamba wanasiasa walikuwa ni Miongoni
mwa watu waliopewa vibali vya kuagiza sukari wakati wengine hata uwezo
wa kuagiza hawana matokeo yake waliwauzia vibali hivyo wafanyabiashara
wakubwa walikuja kutengeneza ‘umonopoli’.
3.Udanganyifu. Sukari iliyokuwa
inaagizwa nje kuna baadhi ilikuwa haina ubora wa kimatumizi ya binadamu
sasa wanachokifanya wafanyabiashara ilikuwa wakiifunga kwenye Mifuko
yenye nembo ya viwanda vya ndani.
4.Kutokuwa na sera madhubuti ya kusimamia uagizwaji wa sukari nje ya nchi.
5. Sukari inayozalishwa kwenye baadhi ya
viwanda imekuwa inauzwa kwa mtu mmoja tu Ambae alikuwa akifanya mchezo
wa kuficha sukari ili bei ipande kutokana uhaba wa sukari kwenye soko
kwa makusudi.
6. Sukari imekosa wa kuisemea sababu
wanasiasa wengi niwafanyabiashara wa hii bidhaa na Wengine wanavibali
vya kuagiza kutoka nje.
No comments:
Post a Comment