Tuesday, 10 May 2016

Kufanya Vibaya kwa Simba nani alaumiwe?

 

 Na Yahya Njenge

Makocha wengi Duniani wapo kwa ajili ya kufukuzwa lakini hawafukuzwi wakiwa wamefanya Mazuri bali hufukuza wakiboronga. Ukiona anaondoka na kafanya makubwa  ujue anaenda kufundisha timu ya taifa ama kapata dili sehemu  nyingine. Simba wamefukuza kocha Anayeitwa Dulan Kerry na kuja Steven Mayanja.

Kery  alikuwa mbishi na msimamo wake ambao ulikuwa na faida kwa soka la bongo kwa Upande mwingine haukuwa na faida, pamoja na yote yaliyo tokea kwake aliwaunganisha Wachezaji kwa namna yake alivyoweza kilicho mponza msimamo wake pamoja na udhaifu Mwingine wa kibinadamu. Alichosaidia ni timu kutokuvurugika japo matokeo hayakuwa Mazuri.

Mayanja amekuja kwa mbwembwe akitokea Coast Union na mkwara mzito alipata matokeo kwa mechi tano mfululizo, kwa mara ya kwanza tangu 2013 timu hiyo haukuwahi kufika kileleni mwa msimamo wa ligi, lakini kwa juhudi na nguvu aliyokuja nayo imeonja japo kukaa Juu ya ligi kwa siku kadhaa.

Mpira wa Tanzania ukiwa mjuaji sana unaharibu, alicho kifanya kuleta nidhamu katika timu Ni jambo la msingi mno lakini sasa limeigharimu timu hiyo. Vijana walikuwa na vipaji vya hali Ya juu na nia ya kucheza soka. Kessy tayari anaenda Yanga hukumu ya Banda haijulikani na Isihaka aliko hakujulikani. Mayanja hapaswi kulaumiwa wachezaji nao pamoja na utoto walipaswa kujiheshimu na kulinda kibarua chao.

No comments:

Post a Comment