Thursday 26 May 2016

Bei ya mafuta yapanda na kupita dola 50 kwa pipa

Bei ya mafuta imepanda hadi zaidi ya dola 50 kwa pipa kwa mara ya kwanza kabisa mwaka huu mwaka 2016 wakati uzalishaji wa chini na kuongozeka kwa mahitaji ya mafuta vikiendelea kuchangia kupanda kwa bei.
 

Kupanda kwa bei ya mafuta kunafuatia takwimu za Marekani zinazoonyesha kushuka kwa uzalishaji hasusan kutokana na moto nchini Canada.
 
Uzalishaji wa mafuta yasiyosafishwa nchini Marekani ulishuka kwa pipa milioni 4.2 .
Uzalishaji wa mafuta yasiyosafishwa nchini Marekani ulishuka kwa pipa milioni 4.2 hadi pipa milioni 537.1 kwa wiki kwa mujibu wa idara ya nishati nchini humo..

Canada ndiye muuzaji mkubwa zaidi wa mafuta kwa Marekani na moto wa msituni katika mikoa iliyo magharibi, ulisababisha kupungua kwa karibu mapipa milioni moja kwa siku.
Mazungumzo ya hivi majuzi kati ya nchi za Opec na Urusi kuhusu kupunguza uzalishaji wa mafuta yamechangia kupanda kwa bei.

No comments:

Post a Comment