Monday 18 December 2017

Takukuru yakanusha kumshikilia Nehemia Mchechu

Image result for Nehemiah Mchechu
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini TAKUKURU imekanusha taarifa zilizosambaa mtandaoni kuwa wanamshikilia aliyekuwa Mkurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa NHC Nehemia Mchechu.
Akiongea na East Africa Television leo, Afisa habari wa TAKUKURU Musa Misalaba amesema wanashangaa taarifa hizo zimetoka wapi na wao kama taasisi hawamshikilii Mkurugenzi huyo aliyesimamishwa na Waziri Lukuvi wiki iliyopita.
“Hizo taarifa sijui zimetoka wapi, lakini sisi hatuna huyo mtu, hatujamkamata saa tunashindwa kuelewa watu wanazusha kwa lengo gani”, amesema Misalaba.
Aidha msemaji huyo ameongeza kuwa wao kama taasisi hawajapokea agizo lolote la kumkamata na kumfanyia uchunguzi ndugu Nehemia Mchechu hivyo hawana sababu ya kumkamata.

Nehemia alisimamishwa kazi na Waziiri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Lukuvi siku ya Jumamosi wiki iliyopita. Jana jioni kwenye mitandao zilisambaa taarifa za kukamatwa kwake ambavyo leo TAKUKURU imekanusha.

No comments:

Post a Comment