Thursday 21 December 2017

Neema ya Maji kwa wakazi wa Wilaya ya Chemba Mkoani Dodoma

Vijijji vya Kwamtoro, Sanzawa na Mangasta vilivyopo Dodoma Wilaya ya Chemba wamepata neema ya Maji safi na salama baada ya mfadhili kutoka Abu Dhabi Bwana Jamal Mohamed kutoa msaada wa visima 4 vya Maji safi na salama kwa wananchi hao.

Bwana Jamal Mohamed alipata ujumbe kuwa Maeneo hayo kunashida ya Maji safi ndipo akaamua kujitolea kuwasaidia wananchi hao kwa kuwachimbia visima 4 vyenye urefu wa mita 150 kwenda chini vyenye thamani ya milion 35 kwa kila kimoja.
Mpaka sasa visima 3 vishakamilika na kimoja ndio kimeanza kuchibwa, Jumla ya msaada huo utagharimu milion 140 za kitanzanai.
Wananchi wameelezea furaha yao juu ya msaada hou nakudai kuwa shida ya maji ilikuwa nitatizo kubwa sana katika maeneo hayo ili kupata maji ili kuwa nilazima utembee kilometa 10 mpaka 15.
Kwa mujibu wa waataalamu wa kuchimba visima wanasema visima hivyo kila kimoja kinatoa lita 15,000 kwa saa na kwa mujibu wa wakazi wa maeneo hayo kutakuwa hakuna tena shida ya maji safi na salama.
Jumla ya visima vyote vitatoa maji lita laki 2 mpaka 3 kwa siku ambazo zitaweza kuhudumia watu zaidi ya 2000 mpya 3000 kwa siku.




No comments:

Post a Comment