Wednesday 6 December 2017

Maandamano ya ACT yaingiwa na vikwazo

 Idara ya vijana ya Chama Cha ACT-Wazalendo imesisitiza kuwa itafanya maandamano yake ya amani yenye lengo la kupinga vitendo vya utumwa wanavyofanyiwa vijana wa Afrika nchini Libya.
Pamoja na kutojibiwa barua yao ambayo wameliandikia jeshi la Polisi kwenye mkoa wa kipolisi Kinondoni kwaajili ya kuomba kibali cha maandamano hayo lakini wamesisitiza kuwa watafanya hivyo
“Polisi Kinondoni wanasema barua yetu ya maandamano ya tarehe 8/12/17 imetumwa KANDA na mpaka sasa majibu hawajaletewa, wanasema tuulizie tena kesho tunapenda kuujulisha umma kuwa ratiba ya maandamano yetu haijabadilika”, imesema Taarifa ya hiyo kutoka idara ya vijana ACT-Wazalendo.
Idara hiyo ya vijana imepanga kuandamana siku ya Ijumaa Disemba 8 kuanzia saa 4 asubuhi ambapo wataanzia eneo la Leaders Club jijini Dar es salaam na kuishia ofisi za Ubalazi wa Libya nchini zilizopo Upanga jijini Dar es salaam na watatumia barabara ya Ali Hassan Mwinyi.

Hivi karibuni nchini Libya kumeibuka vikundi vya watu ambavyo vinafanya biashara ya utumwa kwa baadhi ya wageni wanaoingia nchini humo hususani wale wahamiaji ambao hufika nchini humo kwa lengo la kuvuka na kuelekea barani Ulaya.


No comments:

Post a Comment