Thursday 30 November 2017

Marekani yaitaka dunia kusitisha biashara na Korea Kaskazini


Marekani imetoa wito kwa mataifa mbalimbai kukata uhusiano wake wa kidiplomasia na kibiashara na Korea Kaskazini, ikiwa ni hatua ya kupinga majaribio ya makombora ambayo yamekuwa yakifanywa na taifa hilo.
Balozi wa Marekani Nikki Haley, ametoa pendekezo hilo katika mkutano wa dharura wa baraza la usalama la umoja wa mataifa unaoendelea mjini New York.
Bi. Haley amesema kuwa Rais wa Marekani amemtaka Rais wa China Xi Jinping kusitisha biashara ya mafuta ghafi na Korea Kaskazini, kama sehemu ya kutekeleza hatua ya kuwekewa vikwazo kwa taifa hilo.

Kupitia hatua hii ya kuiwekea vikwazo Korea Kaskazini tunapaswa kusitisha asilimia tisini ya biashara na Korea Kaskazini pamoja na asilimia 30 yamafuta yake.

Mwaka 2003, China ilisitisha kupelekea mafuta Korea Kaskazini ,muda mfupi baadaye taifa hilo likasogea katika meza ya majadiliano.
''Tumefikia hatua ya kuitaka China kuchukua hatua Zaidi katika hili, ni lazima isitishe kuipatia mafuta Korea Kaskazini," alisema Haley.
Wajumbe wa baraza la usalama la umoja wa mataifa wanakutana mjini Ne York kujadili hatua ya Korea kaskazini na majaribio ya makombora ya masafa marefu.

Msemaji wa katibu mkuu wa umoja wa Stéphane Dujarric, amesema kuwa Antonio Guterres, amelaani hatua hiyo Korea Kaskazini na kuongeza kuwa huo ni ukiukaji wa maamuzi ya baraza la usalama la umoja wa mataifa.

No comments:

Post a Comment