Tuesday 2 June 2015

Waziri mkuu mstaafu Frederick Sumaye atangaza nia yakuwania urais kupitia CCM

Waziri mkuu mstaafu wa awamu ya tatu Mheshimiwa Fredericky Sumaye ametangaza nia ya kugombea nafasi ya urasi katika kipindi cha awamu ya tano kwa kuainisha viaumbele kadhaa wa kadha ikiwemo kukuza uchumi, kupambana na rushwa, kulinda viwanda kw akuboresha kilimo pamoja na kunda chombo maalumu na mahakama ya kushughulikia ufisadi na rushwa.
Akihutubia kwenye mkutano wa waandishi wa habari jijini Dar-es-Salaam, waziri mkuu msataafu mheshinmiwa Fredericky Sumaye alianza hotuba yake hiyo kwa kueleza jinsi alivyoshughulikia na matataizo ya wananchi kwa kudhibiti mfumuko wa bei na kupunguza madeni ya ndani na ya nje ya Tanzania.
 
Aidha mheshimiwa Sumaye amesema kuwa kama atapata fursa ya kuteuliwa kuwa mgombea wa nafasi ya uraisi kupitia chama cha mapinduzi CCM, amesema atahakikisha anapunguza pengo kati ya walio nacho na wasio nacho, kulinda muungano kwa kudumisha amani na utulivu nchini, sanjali na kukomesha vitendo vya rushwa na ufisadi serikalini.
 
Waziri mkuu huye ambaye anatumi kauli mbiu ya uongozi bora, komesha rushwa jenga uchumi, anakuwa mwanachama wa saba kupitia chama cha mapinduzi kutangaza nia ya kuwania kuteuliwa na chama cha mapinduzi kupeperusha bendera ya chama hicho kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwaka 2015.
 

No comments:

Post a Comment