Tuesday 16 June 2015

Ajali ya basi, lori yaua 23, yajeruhi 31 Iringa.


Iringa.
Watu 23 wamepoteza maisha na wengine 31 wamejeruhiwa katika ajali ya basi iliyotokea juzi usiku katika eneo la Kinyanambo A wilayani Mufindi, barabara kuu ya Iringa –Mbeya.
 
Akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Iringa Pudenciana Protas, alisema kuwa ajali hiyo ilitokea jana  majira ya 1:45 usiku katika eneo la kinyanambo wilayani hapo.
 
Kamanda Protas alisema kuwa ajali hiyo iliyohusisha gari kampuni ya Another G Express yenye namba za usajiri T.927 CEF na gari ya kampuni ya Bravo Logistic (T) limited yenye namba za T.916 AQM lenye trela namba T.595.
 
Waliokufa na kutambuliwa mpaka sasa ni Lukas Pascal, Brasto Samila, Dickson Luvanda, Albert Silla, Rogers Mdoe, Eva Mbalinga, Hadija Mkoi, Clemence Mtati, Mohamed Kalika, Kastoli Mwakyamba, Damian Myala na Sillo Nziku.
 
Waliojeruhiwa ni Majoline Lupembe (23) mkazi wa Iringa, Veronica Simba (20) mkazi wa Tabora, Shadia Ally (24) mkazi wa Iringa, Mariam Mbise (23) mkazi wa Mafinda, Anita Makwela (24) mkazi wa Kilolo, Benita Sagala (18) mkazi wa Njombe, Bertha Mkoi (27),  Rahel Mavika (18) mkazi wa Mufindi, Selina Fulgence (23) mkazi wa Kigoma na  Maria Mwenda (17) mkazi wa Mafinga.
 
Wengine ni Ndipako Mbilinyi (23) mkazi wa Njombe, Alexander Mkakazii (28) mkazi wa Mafinga, Meshack Kibiki (44) mkazi wa Mafinga, Simon Jumbe (22) mkazi wa Singida, Jerry Lutego (36) mkazi wa Mafinga, Enock Kanyika (18) mkazi wa Mafinga, Deogratius Kayombo (21) mkazi wa Mafinga na Yusuph Lulanda  (22) mkazi wa Njonbe.
 
Wengine ni Petro Mwalongo (21) mkazi wa Njombe, Paulo Chane (21) mkazi wa Kilolo, Kenned Msemwa (28) mkazi wa Njombe, Mode Shiraz (21) mkazi wa Singida, Emmanuel Antony (21) mkazi wa Mwanza, Godfrey Kanyika (39) mkazi wa Mafinga, Boniface Bosha (20) mkazi wa Sumbawanga, Ambiana Meshack (35) mkazi wa Njombe, Martha Kanyika (30) mkazi wa Mafinga, Merina Tonga (miezi miwili), Yusuph Luhamba (34) mkazi wa Mafinga na wanaume wawili na wanawake wawili ambao hawajaweza kutambulika majina yao kutokana na hali zao kuwa mbaya.

No comments:

Post a Comment