Saturday 20 December 2014

ZIARA YA WAZIRI MTWARA


Mhe. Eng. Christopher K. Chiza (MB) Waziri wa Kilimo Chakula na ushirika akikagua ujenzi wa ghala la TANECU (Tandahimba Newala Cooperative Union) Ghala hilo litakuwa na uweza wa kuhifadhi tani 10,000 za korosho na linajengwa Tandahimba . Ghala hilo ni maandalizi ya ujenzi wa kiwanda cha kubangulia korosho kitakachojengwa na TANECU.


Mhe. Eng. Christopher K. Chiza (MB) Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika, akipata maelezo ya zana inayotumika kuandaa mashamba ya mpungaa katika kijiji cha Mahuninga wilaya ya mtwara. Mashamba hayo yenye ukubwa wa ekari 1,000 yanalimwa na mwekezaji mzalendo Bw. Hamis Ismail Msigwa ambaye anashirikiana na vijiji vya Mahuninga na kitunguli.

Mhe. Eng Christopher K. Chiza (MB) akikagua shamba linaloandaliwa kwa ajili ya kilimo cha mpunga katika kijiji cha Mahuninga katka Wilaya ya Mtwara. Mashamba hayo yanamilikiwa na mwekezaji mzalendo Hamis Ismail Msigwa.

No comments:

Post a Comment