Wednesday 29 March 2017

Yanga yapigwa yakataliwa CAF

 Image result for yanga sc
Shirikisho la  Soka Afrika (CAF), limekataa mchezo wa kwanza wa mchujo wa kuwania kuingia hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika kati ya Yanga SC na MC Alger ya Algeria kuchezwa Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza Aprili 8, mwaka huu kutokana na wenyeji kuchelewesha kuthibitisha mabadiliko ya Uwanja.
Uwanja wa nyumbani wa Yanga unaofahamika na waliouthibitisha ni wa Taifa, Dar es Salaam, lakini klabu hiyo ilikuwa katika jitihada za kuuhamishia mchezo huo Mwanza kwa tamaa ya mapato zaidi. 
Hata hivyo, tarehe ya mwisho ya kuwasilisha mabadiliko yoyote ya Uwanja ilikuwa ni juzi wakati Mkaguzi wa CAF, Maxwell Mtonga kutoka Malawi aliupitisha Uwanja huo jana.
Mtonga alikuwa Mwanza tangu juzi akiongozwa na Mkurugenzi wa Ufundi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Salum Madadi katika ukaguzi huo na ameagiza marekebisho madogo madogo.
Meneja wa Uwanja wa CCM Kirumba, Steven Shijja aliahidi kuhakikisha wanafanya marekebisho hayo ndani ya muda kama walivyoelekezwa ili mchezo huo ufanyike Mwanza.
Na tayari mchezo wa Ligi Kuu ya Vodaocm Tanzania Bara kati ya wenyeji Mbao FC na Simba SC ya Dar es Salaam uliokuwa ufanyike Aprili 8, mwaka huu Uwanja wa CCM Kirumba, ulikwishasogezwa mbele kwa siku mbili hadi Aprili, 10.

Yanga SC imeangukia Kombe la Shirikisho Afrika baada ya kutolewa katika michuano ya Ligi ya Mabingwa baada ya sare ya 0-0 na wenyeji, Zanaco Uwanja wa Taifa wa Mashujaa, Lusaka nchini Zambia ikitoka kulazimishwa sare ya 1-1 kwenye mchezo wa kwanza Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Yanga sasa inaweza kucheza Kirumba iwapo tu itafuzu hatua ya makundi na pia watatakiwa kuwasilisha mabadiliko ya Uwanja mapema kwa mujibu wa kanuni.

No comments:

Post a Comment