
Bw Ya'alon amesema Israel imepoteza mwelekeo
Aidha, amesema ataacha kujihusisha na siasa.
Kumekuwa na taarifa kwamba Bw Netanyahu, anapanga kukaribisha chama chenye msimamo mkali kinachoongozwa na Avigdor Lieberman kwenye muungano wake unaotawala.
Bw Lieberman aliwahi kuhudumu kama waziri wa mambo ya nje na anajulikana kwa kutoa matamshi makali na kuwa na msimamo mkali dhidi ya Wapalestina.
Awali Alhamisi, Bw Ya'alon aliwahutubia viongozi vijana wa Israel na kusema taifa hilo limepoteza mwelekeo wake kimaadili.
Taarifa katika vyombo vya habari nchini Israel zinasema Bw Netanyahu atamteua Bw Lieberman kuwa waziri mpya wa ulinzi.

Alishtakiwa lakini baadaye akapatikana bila hatia.
No comments:
Post a Comment