Kaimu Mkurugenzi Idara ya
Maendeleo ya Sanaa wa Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo
Bi.Joyce Hagu akifafanua jambo wakati wa ufunguzi wa semina ya wasanii
wa muziki wa singeli jana Jijini Dar es Salaam,kulia ni Meneja Mkuu wa
EFM Bw.Denis Ssebo na kushoto ni Mkurugenzi wa EFM Bw. Francis Ciza.
Mkuu wa Matukio ya Sanaa wa
Baraza la Sanaa la Taifa(BASATA),Bw.Kuwijira Maregesi akiongea na
waasanii kuhusu maadili ya utunzi wa mashairi wa nyimbo zao wakati wa
ufunguzi wa semina ya wasanii wa muziki wa singeli iliyoandaliwa na
uongozi wa Radio ya EFM jana Jijini Dar es Salaam kushoto ni Afisa Sanaa
Bi. Bona Masenge na kulia ni Mkurugenzi wa Radio EFM Bw.Francis Ciza.
Meneja Mawasiliano wa Mamlaka ya
Mawasiliano Tanzania (TCRA),Bw.Innocent Mungi akiwasisitiza wasanii
(hawapo katika picha) matumizi sahii ya mitandao ya kijamii wakati wa
semina ya wanamuziki wa singeli iliyoandaliwa na uongozi wa Radio ya EFM
jana Jijini Dar es Salaam.
Meneja Elimu kwa Mlipakodi kutoka
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bibi.Valentina Baltaz akiongea kuhusu
umuhimu wa wasanii kulipa kodi kupitia kazi zao za sanaa ili kuchangia
pato la taifa wakati wa semina la wasanii wa muziki wa singeli
iliyoandaliwa na uongozi wa Radio ya EFM jana Jijini Dar es Salaam kulia
ni Mhariri Mkuu wa EFM Bi.Scholastica Mazula.
Afisa Sanaa kutoka Baraza la
Sanaa la Taifa (BASATA) Bi.Bona Masenge akiongea na wasanii(Hawapo
katika Picha) kwa kuwataka kutunza na kuendeleza utamaduni wa kitanzania
kwa kufuata taratibu na sheria katika kazi zao za sanaa wakati wa
semina ya wasanii wa muziki wa singeli leo Jijini Dar es Salaam, kushoto
ni Meneja Mawasiliano wa Taasisi ya Mawasiliano Tanzania
(TCRA),Bw.Innocent Mungi na kulia ni Mkuu wa Matukio ya Sanaa wa Baraza
la Sanaa la Taifa(BASATA),Bw.Kurwijira Maregesi
Baadhi ya Wasanii wa Muziki wa
Singeli waliohudhuria semina iliyoandaliwa na uongozi wa radio EFM kwa
lengo la kuwapata somo la kuifanya sanaa kuwa ujasiliamali ikiwemo
kupata mbinu mbalimbali za uwekezaji .
Baadhi ya Wasanii wa Muziki wa
Singeli waliohudhuria semina iliyoandaliwa na uongozi wa radio EFM kwa
lengo la kuwapata somo la kuifanya sanaa kuwa ujasiliamali ikiwemo
kupata mbinu mbalimbali za uwekezaji .
Kaimu Mkurugenzi Idara ya
Maendeleo ya Sanaa wa Wizara ya Habari Utamaduni,Sanaa na Michezo
Bi.Joyce Hagu(wa tano kutoka kushoto waliokaa) akiwa katika picha ya
pamoja na wasanii wa muziki wa singeli baada ya semina iliyokuwa
imeandaliwa na uongozi wa Radio EFM jana Jijini Dar es Salaam.
Picha na Lorietha Laurence
Na Lorietha Laurence-WHUSM
Wasanii wa Muziki wa Singeli
wameaswa kuzingatia mafunzo ya sanaa ya ujasiliamali yatakayowasaidia
kuongeza weledi na mbinu za kukuza kazi zao na hatimaye kuwa na sanaa
bora kwa ukanda wa Afrika Mashariki.
Hayo yamesemwa na Kaimu
Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Sanaa wa Wizara ya Habari
Utamaduni,Sanaa na Michezo Bi.Joyce Hagu wakati wa ufunguzi wa semina ya
wasanii wa muziki wa singeli jana Jijini Dar es Salaam.
Bi Joyce aliongeza kwa kusema
kuwa sanaa ya muziki ni kazi kama kazi nyingine hivyo ni budi kusimamia
misingi iliyo bora inayoendana na utamaduni wa kitanzania katika utunzi
wa tungo za singeli.
“Utamaduni ni mali ya jamii hivyo
ni jukumu letu sote kupenda,kuthamini na kuendeleza utamaduni wetu
kupitia kazi za sanaa na hii itasaidia kutekeleza kwa vitendo Sera ya
Taifa ya Utamaduni” alisema Bi.Joyce.
Aidha aliupongeza uongozi wa EFM
kwa kuandaa semina hiyo ambayo imewapa fursa wasanii kupata elimu ya
msingi kuhusu muziki na kuifanya kazi ya sanaa kuwa ya thamani kwa
jamii.
Naye Meneja Mawasiliano wa
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA),Bw.Innocent Mungi amewataka
wasanii hao kutumia vizuri mitandao ya kijamii kwa kuuza kazi zao za
mziki na hivyo kuwa na soko la kimataifa na sio kutumia mitandao kwa
ajili ya kuchafuana.
Kwa Upande wake Mkuu wa Matukio
ya Sanaa wa Baraza la Sanaa la Taifa(BASATA),Bw.Kuwijira Maregesi
amewakumbusha wasanii hao umuhimu wa kuzingatia maadili pale
wanapofanya utunzi wa nyimbo zao ili kuepuka usumbufu wa kufungiwa.
Mbali na mada ya maadili wasanii
walipata fursa ya elimu ya mlipa kodi kutoka kwa Meneja Elimu kwa
Mlipakodi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bibi.Valentina Baltaz
ambapo aliwaeleza wasanii umuhimu wa kulipa kodi kupitia kazi zao za
sanaa kulingana na sheria na taratibu za nchi ili kuchangia katika
kukuza pato la taifa.
No comments:
Post a Comment