Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete,ameshiriki katika zoezi la kuchangia damu linalotambulika ‘’Changia Damu Salama kwa Mama na Mtoto’’lilifanyika jimboni humo ili kusaidia upatikanaji wa damu salama.
Akizungumza katika zoezi hilo Ridhiwani amesema kuwa amevutiwa na zoezi hilo na kuamua kujitolea kuchangia damu ili kumkomboa mama na mtoto.Katika tukio lingine Ridhiwani amekutana na kufanya mazungumzo na wakinamama wa jamii ya wafugaji wa kabila la wa Maasai ili kuangalia ni namna gani atasaidia kutatua changamoto zinazowakabili wafugaji katika jimbo hilo.
Aidha amepata nafasi ya kutembelea Lambo la maji lililojaa matope katika eneo la Pera ili kujionea hali halisi ya eneo hilo ili kusaidia kurudisha lambo hilo katika hali yake ya kawaida.
No comments:
Post a Comment