Laizer ambaye ametengeneza hits kadhaa kama ‘Bado’ ya Harmonize na
Diamond, ‘Salome’ ya Diamond pamoja na nyingine nyingi za wasanii wa
WCB, amesema yeye kama producer anaona kila msanii anaimba katika mtindo
wake.
“Binafsi mimi sioni kama Harmonize anaimba kama Diamond,” Laizer
alikimbia kipindi cha FNL cha EATV. “Kwa sababu hata ukisikia ule wimbo
ya ‘Bado’, bado utajua huyu ni Harmonize na yule ni Diamond. Pia labda
ni kwa sababu wanaendana ndiyo maana wanafananishwa lakini kila mtu
anaimba kivyake kabisa,”
Pia mtayarishaji huyo alisema kila msanii wa WCB ana upekee wake katika muziki wake.
No comments:
Post a Comment