Thursday, 21 December 2017

Rais wa orea Kaskazini, Kim Jong Un amepiga marufuku sikukuu ya Krismasi

Pyongyaung. Kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong Un amepiga marufuku mikusanyiko inayoashiria kusherehekea sikukuu ya Krismasi kama vile inayohusu unywaji na uimbaji.
Ametaka wananchi kutosherehekea sikukuu hiyo na wanaopenda kufanya hivyo, waitumie Desemba 24 kusherehekea siku ya kuzaliwa kwa bibi yake aliyezaliwa siku kama hiyo mwaka 1919.
Kiongozi huyo ameviagiza vyombo vya ulinzi na usalama kuhakikisha vinadhibiti mikusanyiko yote ambayo inaendana na maadhimisho ya Krismasi.
“Ni marufuku watu kukusanyika na kufanya mambo kama ya unywaji au kuimba katika sikukuu ya Krismasi,” chanzo kimoja cha habari kimenukuu taarifa ya kiongozi huyo.
Kim Jong Un amekuwa akichukua hatua kuzua kuenea kwa utamaduni kwa kigeni na amedhibiti vyombo vya habari kutotangaza taarifa zozote zinazoienzi sikukuu hiyo kama hatua ya kupiga marufuku Krismasi.

Wednesday, 20 December 2017

ZILIZONOGESHA KURASA ZA MBELE KATIKA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI DESEMBA 21 2017




Rais Magaufuli:Kiama kwa wanaosema vyuma vimekaza kuburuzwa Mahakamani

Rais  Dkt. John Pombe Magufuli amefunguka na kusema kuwa watu ambao wanasema vyuma vimekaza na wale ambao wamekuwa wakisambaza takwimu mbalimbali za kupikwa kukamatwa na kuwekwa ndani na baadaye kupelekwa mahakamani.
Magufuli amesema hayo leo alipokuwa akiweka jiwe la msingi katika jengo la ofisi ya Taifa ya Takwimu Dodoma na kuwataka wananchi kuwa makini na masuala ya takwimu pia amewataka kuwapuuza watu ambao wanasema vyuma vimekaza ili hala watu wa Takwimu wanasema vyuma vimefunguka.

"Ukikosea kutoa takwimu umeichafua nchi, takwimu ni kitu kibaya sana ndiyo maana kuna watu wamebobea kwenye takwimu hivyo wananchi tuwasikilize watu wa takwimu asitokee mtu mwingine akatoa takwimu tofauti na zile walizonazo watu wa takwimu. Mtu anasema vyuma vimekaza wakati watu wa takwimu wanasema vyuma vimefunguka watu hawa wanatakiwa kukamatwa na kuwekwa ndani ili wakajifunze kutoa takwimu huko" alisema Rais Magufuli

Mbali na hilo Rais Magufuli ameagiza watu ambao watatoa taarifa zozote ambazo zipo kinyume na takwimu walizonazo watu wa takwimu wafikishwe mahakamani "Mimi ningekuwa hakimu watu wa namna hiyo wangepewa adhabu zote mbili kulipa faini na kufungwa"

Mbatia alazwa KCMC

Mbunge wa Vunjo (NCCR-Mageuzi), James Mbatia amelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC mjini Moshi baada ya kuvunjika mkono.
Mbatia ambaye pia ni mwenyekiti mwenza wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), amevunjika mkono wa kushoto baada ya kuteleza na kuanguka na amelazwa katika wodi za watu mashuhuri (VIP).
Msaidizi wa mbunge huyo, Hamis Hamis amesema leo Jumatano Desemba 20,2017 kuwa tukio hilo lilitokea jana saa 2:45 usiku wakati akiondoka hotelini kurejea nyumbani.

Hamis amesema Mbatia alikuwa akishuka ngazi katika hoteli ya Uhuru iliyopo eneo la Shanty Town ndipo alipoteleza na kuanguka.
“Bahati nzuri pale kulikuwa na daktari wa KCMC anaiwa Ansbert Sweetbert ndiye alitoa huduma ya kwanza hadi kumpeleka KCMC,” amesema.
Amesema, “Kwa kweli huyo daktari alikuwa msaada mkubwa. Ndiye aliyempeleka KCMC na alikaa naye hadi saa nane usiku. Wauguzi na madaktari KCMC walimpa msaada mkubwa.”
Mbatia ambaye pia ni mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi alipotafutwa leo mchana amesema bado maumivu aliyonayo ni makali kutokana na kuvunjika mkono.
“Bado nina maumivu makali. Nashukuru sana Mungu na jopo la madaktari limeshakutana na watafanya uamuzi,” amesema.

Ronaldo kujenga hospitali ya Watoto Santiago


Nyota wa klabu ya Real Madrid na timu ya taifa ya Ureno Cristiano Ronaldo anatarajia kujenga hospitali ya watoto jijini Santiago nchini Chile.
Hospitali hiyo ambayo itajengwa na Ronaldo akishirikiana na mfanyabiashara kutoka nchini Italia Alessandro Proto, inatarajiwa kukamilika kabla ya mwaka 2020.
Jiji la Santiago umekuwa mji wa kwanza kati ya mingine ambayo Ronaldo na Proto wanampango wa kujenga hospitali hizo za watoto barani Amerika Kusini.
Ronaldo amekuwa mdau mkubwa wa kuchangia damu kwaajili ya watoto wenye matatizo mbalimbali ambapo amefanya hivyo mara kwa mara. Pia nyota huyo ni balozi wa “Save the Children, Unicef ​“ na “World Vision”.

Chelsea kumenyana na Fc Bournamouth

Msimu wa sikukuu za Xmass umefika, na kama kawaida kwa wenzetu barani Ulaya huwa katika kipindi hichi ndio kipindi ambacho timu zinakuwa na mechi nyingi sana, leo tuone jinsi timu kubwa EPL zilivyo na ratiba ngumu.

Manchester United, wametoka kucheza Jpili mchezo wa ligi zidi ya WBA lakini kesho wako uwanjani mchezo wa Carbao Cup vs Bristol na siku tatu baadae watwafuata Leicester City kisha siku tatu baadae watarudi nyumbani kuisubiri Burnley na kisha Southampton tar 30, watapumzika tar 31 na ikifika tareh 1 watakwenda Goodison Park kuikabili Everton kabla ya kucheza na Derby Country siku nne baadae.

Manchester City, hii leo watacheza vs Leicester City ugenini baadae Jumamos watawakaribisha FC Bournamouth kabla ya kuwafuata Newcastle siku tatu baadae kisha watapumzika na baada ya siku tatu Dec 31 watawakabili Crystal Palace na watapumzika siku moja kisha tar 2 January watawaalika Watford  na Jan 6 watakuwa Etihad kuwakabili Burnley.
Chelsea, leo Dec 20 wanawakaribisha Fc Bournamouth kisha Dec 23 watawafuata Everton, Dec 26 watawakaribisha Brighton kisha Dec 30 watawakaribisha Stoke City baada ya hapo watapumzika siku 3 kabla ya kucheza mchezo mgumu ugenini vs Arsenal na Jan 6 watamalizia na Norwich.
Arsenal, hii leo watacheza vs West Ham, na kisha siku ya Ijumaa watawakabili Liverpool wakiwa nyumbani, Dec 28 watawafuata Crystal Palace kisha siku ya mkesha wa mwaka mpya watacheza vs West Brom, wataukaribisha mwaka tar 3 January vs Chelsea kabla ya Jan 7 kukipiga vs Nottinghma Fores.

Tuesday, 19 December 2017

KURASA ZA MAGAZETI YA LEO JUMATANO DISEMBA 20 2017




Aliyekuwa Mwenyekiti wa UVCCM apata Dhamana

 Image result for Sadifa Juma Khamis
Mahakama ya Hakimu Mkazi Dodoma iemwachia kwa dhamana aliyekuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), Sadifa Juma Khamis (Mbunge) anayekabiliwa na mashtaka ya kutoa rushwa wakati wa uchaguzi mkuu wa viongozi wa UVCCM Taifa.
Sadifa ameachiwa leo Desemba 19, 2017 baada ya mahakama kutupilia mbali pingamizi la upande wa mashtaka ambao waliliwasilisha mahakamani hapo kuweka zuio la kupewa dhamana.

Mtuhumiwa huyo ametakiwa kudhaminiwa na watu watatu pamoja na kusaini bondi ya Tsh. Milioni 1, huku akipewa masharti ya kutosafiri nje ya nchi.

Moyes ajisifia uwezo wake wa kufundisha timu


Meneja wa wagonga nyundo wa London West Ham United David Moyes, amesema uwezo alionao kwa sasa anaweza kuifundisha timu yoyote duniani na anataka kuonesha kama ana uwezo huo akiwa na klabu yake ya West Ham United.
Tangu alipoteuliwa  kuwa  kocha wa West Ham United  Moyes, ameisaidia timu hiyo kutoka katika mstari wa timu zinazotakiwa kushuka daraja kwa kutokufungwa michezo mitatu.
"Nina uwezo  wa kufanya kazi hii katika klabu yoyote duniani na nina uhakika nitalifanya hili nikiwa na West Ham," alisema kocha huyo.
Kocha huyo  raia wa Scotland mwenye  umri wa miaka 54, anajaribu kurudisha heshima yake baada ya kufanya vibaya alipoviongoza vilabu vya Manchester United, Real Sociedad na Sunderland.

Marekani yailaumu Korea Kaskazini kwa kirusi cha WannaCry

Utawala nchini Marekani unasema kuwa Korea Kaskazini ilihusika moja kwa moja na kirusi cha wannaCry kilichoadhiri hospitali, biashara na mabenki kote duniani mapema mwaka huu.
Kirusi hicho kilidaiwa kuvamia zaidi ya kampuni 300,000 kwenye mataifa 150 na kusababisha hasara ya mabilioni ya dola.
Thomas Bossert ambaye ni msadizi wa Rais Donald Trump, aliyasema haya kupitia jarida la Wall Street Journal, Hii ndiyo mara ya kwanza Marekani imeilaumu Korea Kaskazimni kwa kirusi hicho.
Bw. Bossert anayemshauri Trump katika masuala ya usalama wa ndani wa nchi alisema kuwa madai hayo ni kutokana na ushahidi uliopo.
Serikali ya Uingereza na kampuni ya kompiuta ya Microsof waliilaumu Korea Kaskazini kwa kirusi hicho.

Trump: China na Urusi ndio washindani wakubwa wa Marekani

Rais Donald Trump ametangaza mkakati wa kitaifa wa usalama katika utawala wake ambao unaangazia vipaumbele vya kwanza vya Marekani.
Mkakati huo umesisitiza ukuaji wa kiuchumi na usalama wa taifa hilo kwa kuweka sheria kali za kulinda mipaka na kuwa na jeshi imara.
Katika hotuba yake,rais Trump ametaja kuwa China na Urusi ni washindani wanaopinga ushawishi wa Marekani katika ngazi ya kimataifa.
Licha ya kuwa Marekani inaongoza kwa kuwa na jeshi lenye nguvu lakini bado wapinzani wake wa kisiasa na kiuchumi wanahangaika duniani kote ili kuitoa katika mstari.
Huku ikiwa inakabiliwa na makundi ya kigaidi ,mitandao ya wahalifu na watu wengine ambao wanachochea vurugu na uovu.
Aidha mkakati huo unajumuisha ujenzi wa ukuta katika mpaka wa Mexico, kuimarisha sheria za uhamiaji na kusitisha mpango wa kutoa viza za bahati nasibu.

Monday, 18 December 2017

MAGAZETI YA LEO JUMANNE DISEMBA 19 2017




Takukuru yakanusha kumshikilia Nehemia Mchechu

Image result for Nehemiah Mchechu
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini TAKUKURU imekanusha taarifa zilizosambaa mtandaoni kuwa wanamshikilia aliyekuwa Mkurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa NHC Nehemia Mchechu.
Akiongea na East Africa Television leo, Afisa habari wa TAKUKURU Musa Misalaba amesema wanashangaa taarifa hizo zimetoka wapi na wao kama taasisi hawamshikilii Mkurugenzi huyo aliyesimamishwa na Waziri Lukuvi wiki iliyopita.
“Hizo taarifa sijui zimetoka wapi, lakini sisi hatuna huyo mtu, hatujamkamata saa tunashindwa kuelewa watu wanazusha kwa lengo gani”, amesema Misalaba.
Aidha msemaji huyo ameongeza kuwa wao kama taasisi hawajapokea agizo lolote la kumkamata na kumfanyia uchunguzi ndugu Nehemia Mchechu hivyo hawana sababu ya kumkamata.

Sheikh Ponda achiwa huru na Mahakama kuu

  Image result for , Sheikh Issa Ponda
Mahakama Kuu ya Tanzania Dar es salaam leo ambapo imeamuachia huru Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu, Sheikh Issa Ponda katika rufaa iliyokatwa na Jamuhuri kupinga Hukumu ya Mahakama ya Morogoro iliyomuachia huru Ponda.
Sheikh Ponda ameachiwa huru mbele ya Jaji Johnson Mkasimongwa ambaye amesema anakubaliana na uamuzi wa Mahakama ya Morogoro kumuachia huru Sheikh Ponda katika kesi ya kutoa matamshi ya uchochezi.
“Mahakama ya Morogoro haikukosea kumuachia huru Sheikh Ponda na mimi nakubaliana na uamuzi huo, hivyo namuachia huru,” – Jaji Mkasimongwa

Miongoni mwa hoja alizozitoa Jaji Mkasimongwa ni kwamba upande Jamhuri haikupaswa kumshtaki Sheikh Ponda kwa kosa lile la kuvunja amri ya Mahakama ya Kisutu bali ilitakiwa wamrudishe katika Mahakama hiyo ili imchukulie hatua zaidi.
Katika mashtaka yaliyokuwa yakimkabiri katika Mahakama ya Morogoro, Sheikh Ponda anadaiwa August 10, 2013, katika eneo la Uwanja wa Ndege, Manispaa ya Morogoro, Ponda aliwaambia Waislamu wasikubali uundwaji wa kamati za ulinzi na usalama za misikiti, kwa madai kuwa zimeundwa na BAKWATA, ambao ni vibaraka wa CCM na serikali.
Pia inadaiwa aliwaagiza waumini hao kuwa endapo watu hao watajitokeza kwao na kujitabulisha kwamba ni kamati za ulinzi na usalama za misikiti, wafunge milango na madirisha wawapige.
Ilielezwa kuwa kauli hiyo ni kinyume cha agizo la Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, iliyotolewa na Hakimu Victoria Nongwa May 9, 2010, ambayo ilimtaka Ponda ndani ya mwaka mzima kuhubiri amani na Kuwa Raia Mwema.

Rais Magufuli:Nimepokea majina mengine ya viongozi wa upinzani ambao wanataka kurudi CCM


Leo Mwenyekiti wa Chama cha  Mapinduzi taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amesema CCM kimekuwa chama imara na chama kinachoendelea kuwavutia watu wengi kila siku ikiwemo viongozi na wanachama kutoka vyama upinzani nchini.
Rais Magufuli amesema kuwa kutokana na uimara wa CCM amepokea majina nane ya madiwani wa vyama vya upinzani na Mbunge mmoja ambapo wanasubiri muda tu kutangazwa.
“Nimepokea majina mengine ya viongozi wa upinzani ambao wanataka kurudi Chama Cha Mapinduzi (CCM) wasaidizi wangu wameniambia yupo Mbunge mmoja anataka kurudi na ameniambia kuwa anataka kuja na madiwani saba kwenye jimbo lake, nasema hiki ni kimbunga na wataisoma namba kweli kweli.“amesema Rais Magufuli leo Desemba 18, 2017, kwenye Mkutano Mkuu wa 9 wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambao unafanyika mjini Dodoma.

Saturday, 16 December 2017

ZILIZOONEKANA KATIKA VYUMBA VYA HABARI KUPITIA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI DISEMBA 17 2017




Mourinho amuweka Bale katika usajili wa mwezi Januari Mwakani

 Image result for Gareth Bale.
Kocha  wa Manchester United, Jose Mourinho anaamini straika wake Zlatan Ibrahimovic aliyerejea uwanjani hataweza kucheza vizuri kama ilivyo-kuwa awali, hivyo yupo mbioni kumsajili Gareth Bale.
Kwa muda mrefu Mourinho amekuwa akihusishwa na mipango ya kumuhitaji Bale kutoka Real Madrid ili akaongeze nguvu ya ushambuliaji katika kikosi chake.

Habari kutoka Man United, zimeeleza kuwa Mourinho anataka kumfanya Bale kuwa usajili muhimu katika usajili ujao wa Januari ili kuimarisha kikosi chake katika Ligi ya Mabingwa Ulaya na Ligi Kuu England.

Awali, ilionekana kama ni vigumu kwa Bale raia wa Wales kutua Man United lakini sasa inaonekana Madrid inaelekea kuchoka kuwa na mshambuliaji huyo ambaye ana majeraha ya mara kwa mara.

Licha ya kuonekana kuwa na nia ya kumuuza, Madrid imeweka dau la pauni milioni 79 kwa Bale japokuwa awali Man United inadaiwa kuweka mkakati wa kutolipa zaidi ya pauni milioni 65 ili kumsajili Bale.

Tottenham Hotspur inaonekana kutaka kuizidi kete Man United, lakini mazungumzo ya mwanzoni mwa msimu huu kati ya Bale na Man United yanampa nafasi Mourinho ya kumnasa mchezaji huyo.

Mourinho anaelezwa kuweka presha ya kumsajili Bale kwa kiasi ambacho Madrid watakitaka huku akibaki na mbadala wa Antonie Griezmann wa Atletico Madrid endapo ishu ya Bale ikibuma.

Samiah Suluhu kuibadilisha Dodoma ya kijani tarehe 21 ya mwezi


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amesema ataanza kampeni rasmi ya kuifanya Dodoma kuwa ya kijani tarehe 21 ya mwezi huu kwa kupanda miti katika mji huo.
Makamu wa Rais ameyasema hayo leo wakati wa hafla fupi ya kumkaribisha rasmi mkoani Dodoma ambapo atakuwa akiishi na kufanya majukumu yake ikiwa sehemu ya azma ya Serikali ya awamu ya Tano ya kuifanya Dodoma Makamo Makuu ya Nchi.
Makamu wa Rais alitoa shukrani za dhati kwa Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa kumrahisishia kuhamia Dodoma pamoja na Waziri Mkuu .
“Tupo Dodoma na Tumehamia rasmi Dodoma, Mwaka mmoja na nusu sasa toka tamko la kuhamia Dodoma limetolewa kuwa ile safari ya Kanani kwa upande wangu leo imetimia”

Kwa upande wake Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa aliielezea siku ya leo kuwa ni siku ya furaha kubwa kwa Watanzania wote haswa wakazi wa Dodoma.
Waziri Mkuu alimuhakikishia Makamu wa Rais kuwa Dodoma ni nzuri, na wana Dodoma wamefarijika sana na sekta za utoaji huduma za jamii zimetanuliwa.
Waziri Mkuu alisema kuwa Dodoma ni rahisi kufikika na wananchi kutoka kona zote za nchi yetu, hivyo fursa zipo nyingi kwa wananchi wa Dodoma na wa mikoa ya jirani.
Waziri Mkuu alianisha barabara kadhaa ambazo zimekamilika kwa kiwango cha lami na zinazorahisisha usafiri kufika Dodoma lakini pia alizungumzia mradi wa reli mpya ya Standard Gauge ambayo itasaidia usafiri kwa muda mfupi kutoka Dodoma kwenda Dar es Salaam.

Msigwa awajia juu wanamshawishi ahamie CCM

 Related image
Mbunge wa Iringa Mjini Mch. Peter Msigwa amewataka wananchi wa Iringa Mjini kumchomea nyumba anayoishi pamoja na magari yake endapo atahama Chama cha Demokrasia na Maendeleo na kuhamia CCM.
Msigwa amefunguka hayo wakati akituma salamu kwa wale ambao wamekuwa wakimrubuni kuhamia CCM na kusema kwamba heshima na dhamana aliyopatiwa na wananchi wa Manispaa ya Iringa ni kubwa mno hivyo kufanya hivyo ni kuuza hadi utu wa wapiga kura.

Msigwa ameweka wazi kwamba amekuwa akipokea simu za vitisho kutoka upande wa chama tawala wakimtaka akubali kupokea ofa yao ya kuhama chama na bila hivyo basi hataweza tena kurudi bungeni baada ya kufika 2020.

"Nikihamia CCM wananchi wa Iringa wachome nyumba yangu  na magari yangu. Sikuingia bungeni kwa sababu nataka hela ila nimeingia kwa sabu kuna hoja kuna agenda na kazi kama chama tunapigania.  Mkome kabisa kunipigia simu mimi sina bei itakayonihamisha CHADEMA," amefunguka Msigwa

Akizungumzia kuhusu alivyokuwa akirubuniwa, Msigwa amesema "Walianza kunipigia kwa kujifanya marafiki zangu na baadae wakaanza kunipanga na kunirubuni kwamba Mzee ananikubali na wala hana shida na mimi hivyo nikiingia CCM nitapata nafasi, nimewakemea na nimeonya wasinipie simu na sasa hivi wameacha ila naahidi wakinipia tena nitawarekodi niwaanike hadharani" I am not that 'cheap' wakatafute wengine," Msigwa ameweka wazi

Aidha Msigwa amefafanua kwamba hakuuingia bungeni kwasababu anahitaji pesa kwani hata kama asingekuwa Mbunge angeweza kuwa Mkurugenzi wa makampuni na kuongeza kwamba  alikuwa na maisha hata kabla ya kuwa mwanasiasa na mbunge.