WADAU wa Sekta binafsi nchini
Jumanne wiki hii, wamefanya mkutano ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya
mkutano wao na serikali chini ya jukwaa la Baraza la Taifa la Biashara
(TNBC) unaotarajiwa kufanyika Mei 6 mwaka huu.
Mkutano huo wa ndani uliandaliwa
na Taasisi ya Sekta binafsi nchini – TPSF ulilenga kuwekana sawa kuhusu
namna bora ya kuiwakilisha sekta binafsi katika mkutano huo muhimu,
ambao Mwenyekiti wake ni Rais wa Jamhuri ya Tanzania Dr. John Pombe
Magufuli.
Akiwakaribisha wadau wa Sekta
Binafsi katika kikao hicho cha maandalizi Mwenyekiti wa TPSF Dk.
Reginald Mengi alisema Serikali na Sekta Binafsi hawakomoani, ndio maana
TPSF inahimiza wafanye kazi kwa pamoja ili kulifikisha taifa kwenye
uchumi wa viwanda.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binafsi nchini (TPSF), Godfrey Simbeye
akitoa neno la ukaribisho kwa wadau wa Sekta Binafsi kwenye mkutano wa
ndani ulioambatana na chakula cha jioni kilichoandaliwa na TPSF katika
hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam. Wa pili kulia ni Mwenyekiti wa
Taasisi ya Sekta Binafsi nchini (TPSF), Dk. Reginald Mengi.
Dk Mengi pia alisema serikali na
sekta binafsi wana malengo yanayofanana ya kutokomeza umaskini na
kutengeneza ajira kwa wananchi, jambo ambalo linaweza kutekelezeka kwa
urahisi iwapo kutakuwa na ushirikiano wa karibu baina ya serikali na
Sekta Binafsi.
Katibu Mtendaji wa TNBC Mhandisi
Raymond Mbilinyi alisema mkutano huo utakuwa ni fursa nzuri kwa serikali
na sekta binafsi kubadilishana mawazo kuhusu wajibu wa kila upande
katika kuboresha mazingira ya biashara na uzalishaji nchini ili kukuza
uchumi wa nchi.
Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) Roberto Jarrin akijitambulisha katika mkutano huo.Mwenyekiti
wa Taasisi ya Sekta Binafsi nchini (TPSF), Dk. Reginald Mengi
akizungumza na wadau wa Sekta Binafsi katika mkutano ulioambatana na
hafla ya chakula cha jioni uliofanyika kwenye hoteli ya Serena jijini
Dar es Salaam. Wa pili kulia ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la
Biashara (TBNC), Mhandisi Raymond Mbilinyi.Mwenyekiti
wa Taasisi ya Sekta Binafsi nchini (TPSF), Dk. Reginald Mengi
akiendelea na mazungumzo na wadau wa Sekta Binafsi kwenye mkutano huo
ulioambatana na chakula cha jioni katika hoteli ya Serena jijini Dar es
Salaam.Katibu
Mtendaji wa Baraza la Taifa la Biashara (TBNC), Mhandisi Raymond
Mbilinyi akifafanua jambo katika mkutano wa ndani ambao ni sehemu ya
kujiandaa kukutana na serikali chini ya Baraza la Taifa la Biashara
(TBNC) linalotarajiwa kufanyika mwanzoni mwa mwezi Mei jijini Dar es
Salaam.Mwenyekiti
wa Taasisi ya Sekta Binafsi nchini (TPSF), Dk. Reginald Mengi akiteta
jambo na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binafsi nchini (TPSF),
Godfrey Simbeye wakati mkutano huo ukiendelea.Mkutano ukiendelea.
No comments:
Post a Comment