
Na Nechi Makundi
Wilaya nne za Ngorongoro,
Karatu,Monduli na Longido,mkoani Arusha, zimekubaliana kuingia katika
mradi wa kitalii wa kuhifadhi na kuendeleza maeneo yenye urithi wa
kijiolojia(Geopark).
Mradi huo, unaoratibiwa na
Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro(NCAA) unategemewa kuwa kivutio kikubwa
cha watalii na watafiti na utasaidia pia kuendeleza jamii zilizo na
maeneo hayo.
Mkurugenzi wa idara ya mambo ya
kale, Donatus kamamba akizungumza katika semina ya kuanzisha mradi huo,
ambayo ilishirikisha wakuu wa wilaya hizo na wenyeviti wa halmashauri,
alisema mradi huo ukianza utakuwa na manufaa makubwa kwa taifa.
Alisema mradi huo,utasaidia sana
kuhifadhi rasilimali zote za kijiolojia, kihistoria na kitamaduni katika
wilaya hizo hivyo kutoa fursa za ajira kwa wananchi.
Wakizungumzia mradi huo, Mkuu wa
wilaya ya Longido Ernest Kahindi na Mkuu wa wilaya ya Ngorongoro,Hashimu
Mgandilwa walisema wanaimani wananchi wa wilaya zao kunufaika na mradi
huo.
Kahindi alisema wilaya ya
Longido, ambayo ina maeneo ya kijiolojia ambayo ni muhimu katika utalii,
itaweza sasa kupata fedha za kigeni katika kuhifadhi maeneo hayo.
Kwa upande wake Mgandilwa alisema
wilaya ya Ngorongoro yenye maeneo kama Mlima oldonyolengai,
inatarajiwa kunufaika kwani miradi itakuwa inasimamiwa na wananchi.
Mwenyeviti wa halmashauri ya
Karatu, Jubilate Mnyenye na Mwenyekiti wa halmashauri ya Monduli, Isack
Joseph walisema mradi wa Geopark ni fursa mpya kwa wananchi.
Mnyenye alisema wilaya ya karatu
ambayo ina maeneo menji ya urithi wa kijiolojia ziwa eyasi na mengine
sasa inatarajia kuendelezwa maeneo hayo.
kwa upande wake Mwenyekiti wa
Monduli, alisema ni wazi fursa ya mradi wa Geopark ikitumiwa vyema
ibadili masisha ya wananchi wake na kuongeza mapato kwa halmashauri.
Mratibu wa mradi huo Mhandisi
Joshua Mwankunda alisema mradi huo, hutolewa na shirika la umoja wa
mataifa la utamaduni (UNESCO) baada ya kukidhi vigezo vinavyotakiwa.
Alisema baada ya kupata hadhi ya
geopark maeneo hayo hujiunga na mtandao wa kidunia wa maeneo ya
Geopark na hivyo kuvutia watalii na watafiti.
No comments:
Post a Comment