Friday, 11 March 2016

Serikali imesitisha Hati za Mashamba Wilayani Monduli


Coffee land for sale
Na Nechi Makundi
 
SERIKALI imefuta hati za mashamba makubwa 13,ambayo kwa muda mrefu yamekuwa Hayaendelezwi  na kuyakabidhi kwa uongozi wa wilaya ya Monduli ili yagawiwe kwa wananchi ambao hawana ardhi.
 
Shughuli hiyo ya kukabidhi mashamba hayo imefanyika kwenye kata mbili za Lokisale na Olmot ,wilayani Monduli, kwenye mkutano wa hadhara .
Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya makazi Wiliam Lukuvi, amesema mashamba hayo yalikuwa Yakimilikiwa na wawekezaji ambao hawayajaendeleza kwa kipindi kirefu yapo vijiji vya Mswakini na Lokisale.
 
Aidha waziri Lukuvi ameuagiza uongozi wa halmashauri ya Monduli, kumpatia orodha ya mashamba mengine 39,ambayo hayajaendelezwa kabla ya mwosho wa Marchi mwaka huu  ili nayo yafutiwe hati  na kuyagawa kwa wananchi ambao hawana mashamba  wilayani humo.
Waziri Lukuvi, amesema kuwa serikali inawahitaji wawekezaji  wa kweli ambao watayaendeleza Maeneo lakini sio ambao wameyatelekeza mashamba hguku wananchi wakikosa mashamba ya kulima .
 
Waziri, Lukuvi,amesema uwekezaji kwenye mashamba lazima uambatane na utoaji wa ajira za kudumu na sio vibarua na ajira iwe ni  chanzo muhimu na kusisitiza wawekezaji ambao hawataki kutoa ajira warudishe ardhi hiyo waliyoimiliki.
 
Amewaambia kuwa ardhi ambayo mwekezaji ameshindwa kuiendeleza ikifutiwa umiliki wake haitalipwa fidia kwa kuwa mhusika ameshindwa kuiendeleza na ameitelekeza.
Waziri, amesisitiza kuwa kipaumbele cha ardhi inayofutiwa hati miliki ni kwa wananchi maskini na Sio wenye uwezo, wenye ardhi au viongozi la hasha bali kipaumbele ni kwa wale ambao hawana kabisa ardhi.
 
Aidha amezuia maafisa ardhi ngazi za kanda nchini kutokujihusisha  na uhamishaji wa umiliki wa Ardhi na mashamba au kusajili mashamba mapya na kutoa hati miliki mpaka waziri ataarifiwe kwanza.
 
Amesema amegundua kuna ujanja ujanja, unaotumiwa na wamiliki wa mashamba ambao huyauza na kusajili maeneo yaliyobakia jambo ambalo ni kinyume na sheria.

No comments:

Post a Comment