
Kochawa Yanga, Mzambia George Lwandamina amesema kwamba ataingia kwenye
mchezo wa leo dhidi ya mahasimu, Simba hali ya kikosi chake ikiwa si
nzuri sana.
Lwandamina amesema kwamba wachezaji wake wanne tegemeo wote ni majeruhi na hawawezi kucheza leo.
Lwandamina amewataja wachezaji majeruhi ni Wazambia wenzake, viungo
Justin Zulu na Obrey Chirwa na washambuliaji Mrundi Amissi Tambwe na
Mzimbabwe Donald Ngoma.
George Lwandamina amesema wachezaji wake tegemeo wanne ni majeruhi kuelekea mchezo wa leo
Pamoja na hao, Lwandamina alisema beki Pato Ngonyani na mshambuliaji
Matheo Anthony nao wote ni wagonjwa na hawana uhakika wa kucheza kesho.
Kwa ujumla Lwandamina ambaye timu yake ilifungwa 4-0 na Azam FC Jumamosi
kwenye mchezo wa mwisho wa Kundi A, alisema ataingia kwenye mchezo wa
kesho katika mazingira magumu ya kukatisha tamaa.
“Lakini hatuna namna nyingine, lazima tuingize timu
tukapambane,”alisema. Yanga inakutana na mahasimu, Simba katika Nusu
Fainali ya Kombe la Mapinduzi usiku wa leo Uwanja wa Amaan, Zanzibar.
No comments:
Post a Comment