
Polisi
wamelazimika kufyatua risasi na mabomu ya kutoa machozi kwa
waandamanaji waliokaribia makao ya rais katika mji muu wa Bujumbura
Burundi.
Mwandishi wa BBC aliyeko huko Maud Jullien amesema kuwa
mamia ya waandamanaji walikuwa takriban kilomita moja kutoka kwa kasri
ya rais ndipo wakavamiwa na maafisa wa usalama.
Viongozi wa kanda ya Afrika Mashariki na kati wanakutana hii leo mjini Dar es Salaam kujadili mbinu za kutatua mgogoro wa kisiasa ambao inalaumiwa kwa kusababisha vifo vya watu 20.
Mkutano huo utakuwa chini ya uenyekiti wa Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete, aliyeuitisha baada ya ujumbe wa mawaziri wa mambo ya nchi za nje wa Jumuiya hiyo, kwenda Bujumbura wiki iliyopita.

Viongozi hao wanatarajiwa kumshinikiza rais Nkurunzinza kuahirisha uchaguzi unaotarajiwa kufanyika mwezi juni.
No comments:
Post a Comment