Sunday, 12 March 2017

Sir. George, Kahama amefariki dunia

Clement George Kahama, al-maarufu Sir. George, mmoja kati ya waasisi wa Taifa la Tanzania Amefariki dunia jioni ya leo katika Hospitali ya Muhimbili Jijini Dar es Salaam.
Clement George Kahama, al-maarufu Sir. George enzi za uhai wake

Aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na Kada wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Balozi Juma Mwapachu amethibitisha kutokea kwa kifo cha Sir. George na kusema kuwa amefariki leo saa kumi na dakika arobaini za jioni. 
Sir. George, ni mtumishi wa umma aliyekuwa mtendaji mkuu na mwanasiasa aliye mahiri na makini, katika utendaji kazi kuanzia nyakati za Tanganyika kudai uhuru mnamo miaka ya 1950, hadi kujitawala mwaka 1961.

Enzi za uhai wake Sir. George alishawahi kuwa waziri katika wizara mbalimbali kwa nyakati tofauti tofauti. Mungu ampumzishe mahali pema peponi.

No comments:

Post a Comment