Friday, 13 January 2017

Kikao cha kujadili changamoto za Muungano

OTI 1
Kikao cha kujadili changamoto za Muungano kinafanyika katika Ukumbi wa zamani wa Baraza la wawakilishi Kikwajuni Unguja. Kikao hiki cha ngazi ya Mawaziri kinajumuisha Mawaziri kutoka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (SMT) na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ). Kikao hicho ni utangulizi wa Kikao cha Makamu wa Rais kitakachofanyika mchana  wa leo.
OTI
Wa pili kutoka kulia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais wa jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. January Makamba, akiongea katika kikao cha ngazi ya Mawaziri kinachohusisha Mawaziri Kutoka Serikali ya Jamhuri ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, kinachojadili changamoto za Muungano, Mjini Unguja, wa Pili kutoka Kushoto ni  Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa (SMZ) Mhe. Mohamed Aboud Mohamed. Kulia kwake ni Bwana Joseph Abdallah Meza Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais (SMZ) na wa kwanza Kulia ni Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muugano wa Tanzania Profesa Faustin Kamuzora.
OTI 2
Katika Picha Sehemu wa viongozi wa Serikali ya (SMZ) katika kikao cha ngazi ya Mawaziri kinachojadili changamoto cha Muungano Mjini Zanzibar Leo.
(Picha na Evelyn Mkokoi na Lulu Mussa wa OMR)

No comments:

Post a Comment