
Rais Dkt. John Pombe Magufuli
akisalimiana na Waziri Mkuu mstaafu, Fredrick Sumaye wakati wa shughuli
za kuagwa kwa mwili wa aliyekuwa kuwa Waziri wa zamani wa Serikali,
Joseph Mungai aliyeagwa leo katika ukumbi wa karimjee Jijini Dar es
Salaam.

Rais Dkt. John Pombe (wa tatu
kulia) akiwa katika ibada maalum ya kumwombea aliyewahi kuwa Waziri wa
zamani wa Serikali, Joseph Mungai aliyeagwa leo katika ukumbi wa
karimjee Jijini Dar es Salaam.

Familia ya Hayati, Joseph Mungai
wakifuatilia kwa makini shughuli za kuagwa kwa mwili wa Waziri huyo wa
zamani wa Serikali zilizofanyika leo katika ukumbi wa karimjee Jijini
Dar es Salaam.

Rais Dkt. John Pombe Magufuli
akitoa salamu za mwisho kwa mwili wa aliyewahi kuwa Waziri wa zamani wa
Serikali, Joseph Mungai aliyeagwa leo katika ukumbi wa karimjee Jijini
Dar es Salaam.

Makamu wa Rais mstaafu, Dkt.
Mohammed Gharib Bilal akitoa salamu za mwisho kwa mwili wa aliyewahi
kuwa Waziri wa zamani wa Serikali, Joseph Mungai aliyeagwa leo katika
ukumbi wa karimjee Jijini Dar es Salaam.

Waziri Mkuu mstaafu, Jaji Joseph
Warioba akitoa salamu za mwisho kwa mwili wa aliyewahi kuwa Waziri wa
zamani wa Serikali, Joseph Mungai aliyeagwa leo katika ukumbi wa
karimjee Jijini Dar es Salaam.

Waziri Mkuu mstaafu, Fredrick
Sumaye akitoa salamu za mwisho kwa mwili wa aliyewahi kuwa Waziri wa
zamani wa Serikali, Joseph Mungai aliyeagwa leo katika ukumbi wa
karimjee Jijini Dar es Salaam.

Waombolezaji wakipita katika
jeneza la aliyewahi kuwa Waziri wa zamani wa Serikali, Joseph Mungai
wakati wa shughuli za kuagwa kwa mwili wa Kiongozi huyo leo Jijini Dar
es Salaam.

Rais mstaafu, Benjamin Mkapa
akibadilishana mawazo na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji
Damian Lubuva wakati wa shughuli za kuagwa kwa mwili wa aliyekuwa kuwa
Waziri wa zamani wa Serikali, Joseph Mungai aliyeagwa leo katika ukumbi
wa karimjee Jijini Dar es Salaam.

Baadhi ya Viongozi waandamizi
kutoka Chama cha Mapinduzi (CCM) na UKAWA wakifuatilia shughuli za
kuagwa kwa mwili wa aliyekuwa Waziri wa zamani wa Serikali, Joseph
Mungai aliyeagwa leo katika ukumbi wa karimjee Jijini Dar es Salaam.
NA IMMACULATE MAKILIKA- MAELEZO
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Mheshimiwa John Magufuli leo ameongoza viongozi mbalimbali
pamoja na umma wa watanzania katika shughuli ya kuaga mwili wa
marehemu John Mungai katika viwanja vya Karim jee vilivyopo jijini Dar
es salaam.
Akizungumza kwa niaba ya Serikali
wakati wa shughuli ya kuaga mwili wa marehemu, Waziri wa Mambo ya Nje
na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Augustine Mahiga alisema
kuwa marehemu Joseph Mungai alikuwa na kipaji cha pekee cha uongozi kwa
vile alipewa madaraka makubwa katika umri mdogo na katika wakati mgumu
katika historia ya nchi.
“Baada tu ya Azimio la Arusha
mwaka 1967 aliyekuwa Rais wa Awamu ya kwanza Mwl. Julius Nyerere
alimteua marehemu Mungai kuwa Waziri wa Kilimo wakati ambao kulikua na
falsafa za siasa ni kilimo na kilimo ni uti wa mgongo, hakika Mwl.
Nyerere alimuona ni kiongozi aliyefaa” alisema Balozi Mahiga
Ameongeza marehemu amejionesha
katika ustawi wa jamii kwa kufanya shughuli mbalimbali za maendeleo ya
jamii pamoja na kusaidia kaya masikini.
Kwa upande wake, mwanasiasa
mkongwe nchini Kingunge Ngombale Mwiru alisema kuwa marehemu Mungai
alikuwa kiongozi mahiri na mzalendo, ambaye alijenga shule za sekondari
zaidi ya saba huko mkoani Iringa ambapo baadae alizikabidhi Serikalini
kwa maendeleo ya Taifa.
Naye msemaji wa Serikali ambaye
ni mtoto wa marehemu Bw. Jimmy Mungai kwa niaba ya familia ameishukuru
Serikali, viongozi mbalimbali pamoja na wananchi kwa kuendelea
kuwafariji katika kipindi hiki kigumu.
Marehemu Joseph Mungai amefariki
Dunia ghafla Novemba 8, mwaka huu na aliwahi kushika nyazifa
mbalimbali serikalini ikiwemo uwaziri kwa awamu nne za serikali, pia
alichaguliwa kuwa mbunge akiwa na miaka 26 na kuwa mbunge mwenye umri
mdogo kuliko wabunge wote wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Viongozi mbalimbali akiwemo Rais
Mstaafu wa Awamu ya Tatu mheshimiwa Benjamini Mkapa, Waziri Mkuu
Mstaafu Fredrick Sumaye, Makamu Mwenyeliti wa Chama cha Mapinduzi Bara
Mheshimiwa Philip Mangula na Spika wa Bunge Mstaafu Mheshimiwa Pius
Msekwa walijumuika kuaga mwili wa marehemu Joseph Mungai
utakaosafirishwa kesho kuelekea mkoani Iringa na kuzikwa jumamosi saa
nane mchana.
No comments:
Post a Comment