Thursday 13 July 2017

Balozi Mwapachu Achia Ngazi Ujumbe wa Acacia

Balozi Juma Mwapachu Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa kampuni ya uchimbaji ya Acacia, ameachia  nafasi hiyo baada ya kuitumikia kwa vipindi viwili.
Mwapachu amechia nafasi hiyo Tarehe 13 Jalai Mwaka huu amechukua uamuzi huo leo, Julai 13 baada ya muhula wake wa pili wa miaka mitatu mitatu wa ujumbe wa bodi hiyo, kumalizika.
Taarifa iliyotumwa leo na Bodi ya Wakurugenzi na Menejimenti ya Acacia imeeleza kuwa inamshukuru Balozi Mwapachu kwa utendaji wake na ushirikiano wake wote  alipokuwa mjumbe.
“Tunamtakia maisha mema,” imesema taarifa hiyo.

No comments:

Post a Comment