Thursday 13 July 2017

Aveva na Kaburu kusota Rumande mpaka Tarehe 20 Julai mwaka huu


Dhamana ya Rais wa Klabu ya Simba, Evans Aveva na Makamu wake, Geofrey Nyange 'Kaburu' imeota mbawa
watuhumiwa hao wenye kesi ya kughushi nyaraka pamoja na kutakatisha Fedha wataendelea kusota Rumande mpaka Tarehe  20  Julai mwaka huu Upelelezi wa Kesi hiyo utakapokamilika utakapokamilika.
Uamuzi huo umetolewa na Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Kisutu Jijini Dar es Salaam, Victoria Nongwa ambapo washtakiwa hao wanakabiliwa na mashtaka matano ambayo mawili kati ya hayo ni ya kutakatisha fedha.

Kutokana na kesi yao ya utakatishaji fedha kutokuwa na dhamana watuhumiwa hao wamerudishwa rumande kwa mara nyingine tena mpaka uchunguzi wa kesi yao utakapokamilika na kupandishwa tena Mahakamani Julai 20 mwaka huu

No comments:

Post a Comment