Saturday 21 October 2017

Zitto atoa Msimamo wa ACT wazalendo

Kiongozi wa chama cha ACT wazalendo Zitto kabwe amesema kuwa chama hicho kinatekeleza wajibu wa sheria ambao upo kikatiba ya Tanzania tofauti na watu wanaosema kwamba wanafanya siasa ya uharakati.
Anasema hayo leo jijini Dar es salaam na waandishi wa habari na kusema kuwa ACT ni chama kinachofanya siasa safi kwa kutetea haki za raia na kupinga uvunjwaji wa katiba ya Tanzania ikiwemo miswada mbalimbali ambao inapelekwa ili kuminya uhuru wa raia.
Zitto aliongeza kwa kusema chama hiki hakitasifia chama tawala hata siku Kama kuna mwanachama yoyote ambae atafikiri tutakisifia akae pembeni Kama walivyokaa pembeni wengine.

No comments:

Post a Comment