Saturday 21 October 2017

Ijue Rekodi ya Mesi

Nyota Lionel Messi wa FC Barcelona si mgeni kwako lakini inawezekana kuna rekodi zake hukuwahi kuzisikia. Hizi hapa nakuwekea...
REKODI ZA MESSI:
2011/12 alifunga mabao 50 katika La Liga, hiyo ni rekodi.
Katika La Liga amefunga mabao 359 ambayo ni idadi ya juu zaidi kuliko mchezaji yoyote.
Katika ngazi ya klabu, Messi ni mchezaji aliyeshinda makombe mengi zaidi yanayotambulika maana ana 29.
Mabao mengi zaidi kwa msimu mmoja kwa michuano yote anaishikilia yeye akiwa na mabao 91.

Pamoja na kuwa hajawahi kubeba Kombe la Dunia, Messi ndiye mchezaji mwenye mabao mengi zaidi timu ya taifa ya Argentina baada ya kupachika 61.

No comments:

Post a Comment