Monday 16 October 2017

Catalonia na uhuru waelekea Mwishoni

 
Kiongozi wa eneo la Catalonia amesalia na saa chache kabla ya kumalizika muda wa mwisho uliowekwa na serikali kuu kuthibitisha wazi ikiwa ametangaza uhuru au la.
Ikiwa atakiri kuwa ametangaza, atakuwa na hadi Alhamisi kufuta tangazo hilo au Catalonia ambayo imekuwa ikijisimamia iongozwe moja kwa moja na Uhispania, Tarehe ya mwisho iliyotolewa kwa Carles Puigdemont ni leo 08:00 GMT.

Baada ya kura ya maoni ya uhuru wiki mbili zilizopita ambayo ilitangazwa kuwa iliyo kinyume na sheria na mahakama ya katiba ya nchi hiyo, Bw Puigdemont alisaini tangazo la uhuru lakini akafuta kutekelezwa kwake, Alisema alitaka mazungumzo na serikali ya Madris lakini hilo halijafanyika.

No comments:

Post a Comment