Thursday 26 October 2017

Mafuriko Dar hatari kubwa

Mvua ya inayoendelea kunyesha kwa siku mbili mfululizo katika jiji la Dar es salaam, imesababisha mafuriko makubwa katika maeneo mbalimbali Jijini humo, ikiwemo eneo la Jangwani ambapo maji hayo yamefunga mawasiliano ya barabara ya Morogoro, Hakuna gari inayokwenda wala kurudi mjini.
Mpaka sasa umeripotiwa kuokotwa katika mto kenge uliopo Tabata jijini humo, mwili wa mtu mmoja mwenye jinsia ya kiume.
Mkuu wa wilaya ya Ilala Sophia Mjema amefika katika eneo hilo nakuwataka wananchi kuondoka katika maeneo hayo kwasasa kwakuwa maji yanaendelea kuongezeka.
Wakaazi wa eneo la Jangwani wakiwa wanaendelea kuopoa baadhi ya mali zao
Abiria wakiwemo Wanafunzi wakiwa wamekwama katika kituo cha mabasi yaendayo haraka cha Jangwani, Dsm.


Mkuu wa wilaya ya Ilala Sophia Mjema amefika katika eneo hilo nakuwataka wananchi kuondoka katika maeneo hayo kwasasa kwakuwa maji yanaendelea kuongezeka.

Mbunge wa Ilala Musa Zungu amefika na kueleza kuwa mafuriko hayo ni makubwa ingawa mpaka sasa hawajapata takwimu sahihi ya uharibifu unaotokana na mafuriko hayo.

No comments:

Post a Comment