Saturday 28 October 2017

Polisi wawili wauawa kwa kupigwa risasi

Polisi wawili waliokuwa kituo cha Polisi Kayole Nairobi wameuawa kwa kupigwa risasi na kisha wauaji kuondoka na bastola walizokuwa nazo
Maafisa polisi wenzake kutoka kambi ya polisi ya Kirima waliikuta miili yao barabarani asubuhi ya leo
Mafisa hao wametambuliwa kuwa ni Konstebo Linus Inima and James Gitahi.
Maafisa wa polisi wamekuwa wakipambana na waandamanaji wanaopinga uchaguzi na eneo la Kayole huko Nairobi ni kati ya maeneo yaliyoathiriwa na vurugu hizo, ila haijajulikana kama mauaji ya polisi hao yanahusiana na uchaguzi

No comments:

Post a Comment