
Mataifa 6 waanzilishi wa Muungano wa
Ulaya EU wanakutana leo kujadili mustakabali wao wa baadaye baada ya
Uingereza kuamua kujiondoa kutoka kwa muungano huo.
Mawaziri wa
mambo ya nje wa Ujerumani, ufaransa,Italy, Ubelgiji, Luxembourg na
Uholanzi wanatarajiwa kuanzisha mchakato huo pasi na kuwa na ngoja
ngoja.Tayari rais wa tume ya muungano wa Ulaya , Jean-Claude Juncker, amesema anataka kuanzisha majadiliano mara moja ya jinsi Uingereza

Mawaziri hao pia wanatarajiwa kuweka masharti mapya yatakayowazuia wanachama wengine kuiga mfano wa Uingereza,baada ya vyama vya mrengo wa kulia katika mataifa mengi duniani kupongeza uamuzi huo wa Uingereza kujitoa kutoka muungano wa Ulaya...

Ameomba kuwepo kwa subra na umakini katika kulishughulikia swala hilo ambalo anasema linapaswa kuongozwa tu na vipi kushughulikia mahitaji ya raia wa jumuiya ya muungano wa Ulaya.
No comments:
Post a Comment